Janga, Au Maafa)
Alipotaka (صلى الله عليه وآله وسلم) kuomba dhidi ya mtu, au kumuombea mtu, alifanya Qunuut ([1]) katika Rak’ah ya mwisho baada ya rukuu, na baada ya kusema: 'Sami'a Allaahu Liman Hamidah, Allaahumma Rabbana lakal Hamd’([2]) "Aliomba kwa sauti"([3]) "alinyanyua mikono"([4]) "ya walionyuma yake walisema Aamiyn"([5])
"Alikuwa akifanya Qunuut katika Swalah zote tano"([6])lakini "hakuwa akifanya Qunuut humo ispokuwa alipoomba dhidi ya watu au kuwaombea watu"([7]) Mfano, mara alisema: ((Ee Allaah! Muokoe Al-Waliyd Ibn Al-Waliyd na Salamah Ibn Hishaam na 'Ayyaash Ibn Abi Rabiy'ah. Ee Allaah! Zidisha adhabu Yako kwa (kabila la) Mudhwar, na wajalie miaka (ya ukame) kama miaka ya Yuusuf. [Ee Allaah! Malaani Lahyaan na Ru'lan, na Dhakwaan, na 'Uswayyah waliomuasi Allaah na Mjumbe Wake]))([8])
Kisha "alikuwa akisema: 'Allaahu Akbar' anapomaliza Qunuut na kusujudu"([9])
[1] "Qunuut" inabeba maana nyingi kama unyenyekevu na uchaji. Na
[2] Al-Bukhaariy na Ahmad.
[3] Kifungu kile kile kilichotajwa hapo mbeleni.
[4] Ahmad na Atw-Twabaraaniy ikiwa na isnaad Swahiyh. Kunyanyua
[5] Abu Daawuud na Siraaj. Al-Haakim amekiri ni Swahiyh, na Adh-Dhahabiy na wengineo wamekubali.
[6] Abu Daawuud, Siraj na Ad-Daaraqutniy ikiwa na isnaad mbili Hasan.
[7] Abu Khuzaymah katika Swahiyh yake (1/78/2) na Al-Khatwiyb katika Kitabu Al-Qunuut ikiwa na isnaad Swahiyh.
[8] Al-Bukhaariy na Ahmad, ziada kutoka kwa Muslim.
[9] An-Nasaaiy, Ahmad, Siraaj (109/1) na Abu Ya'laa katika Musnad yake ikiwa na isnaad nzuri.
0 Comments