Nini Udhu?
Kilugha udhu ni unadhifu, au
kujinadhifisha; Kisharia ni kutumia maji kwenye viungo maalum kwa kuanzia nia
na kuwa khaasa kwa viungo hivyo.
Kuthibiti Kuamrishwa Udhu
Udhu umeamarishwa kwa Qauli ya
Mwenyezi Mungu Mtukufu:
“Enyi mlio amini! Mnapo simama
kwa ajili ya Sala basi osheni nyuso zenu, na mikono yenu mpaka vifundo, na
mpake vichwa vyenu, na osheni miguu yenu mpaka vifundo.........". (Al
Maida : 6).
Shuruti, Fardhi, Sunna na Yenye Kuba'tilisha Udhu
Udhu una shuruti zake, fardhi
zake, suna zake, na una yale yenye kuba'tlisha udhu.
Shuruti za Udhu
Shuruti za kusihi udhu ni kuwa
Muislam, mukalaf, yaani baalegh na mwenye akili timam, maji yawe yenye kujuzu
ku'tahirishia, kutokuwepo juu ya sehemu ya kiungo cha udhu kitu kinachozuia
maji kufika kwenye ngozi ya sehemu hio ya kiwiliwili, na kutokuwa ndani ya
hedhi au nifasi.
Vilevile kwa yule mwenye
maradhi kama vile damu ya (hedhi) ya kudumu, kikojozi, au kujamba, wao
inashurutishwa kuingia wakati wa ile Sala wanayotaka kuisali ndio watie udhu,
sio kabla yake. Hivi ni kwa sababu udhu wa watu hawa ni udhu wa dharura, si
udhu wa kawaida; na kusihi udhu wa dharura sharti yake ni kufika wakati wa lile
la dharura nalo ni wakati wa ile Sala anayotaka kuisali.
Fardhi za Udhu
Fardhi za udhu ni sita:
Ya
Kwanza, kutia nia; hivi ni kutokana na Hadithi ya Mtume wetu Mpenzi
s.a.w.:
“Hakika (kusihi) ibada ni kwa (kupatikana)
nia”. (Imehadithiwa na Al Sheikhan).
Wakati wa kutia nia ni pale
unapoosha sehemu ya mwanzo ya uso huku ukikusudia kuondoa hadathi ndogo
au kujuzu kusali,
au kutekeleza fardhi ya udhu
.
Ya
Pili, kuosha uso; kulingana na Qauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu: “……..osheni nyuso zenu,” (Al Maaida :
6).
Uso kwa urefu ni tangu maoteo
ya nywele mpaka kidevu, na kwa upana ni tangu sikio mpaka sikio. Kuosha uso ni
kuosha kila sehemu ya uso pamoja na nywele ziliomo pembezoni mwa uso na
kidevuni. Ikiwa ni chache hizo nywele yaani inabainika ngozi, basi ni lazima
kufikisha maji mpaka kwenye ngozi, ama ikiwa ni nyingi basi hutosha kwa kupaka
maji juu yake.
Ya
Tatu, kuosha mikono miwili pamoja na vifundo viwili; kulingana na
Qauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu: “..na mikono yenu mpaka
vifundo…” (Al Maaida : 6). Neno mpaka maana yake ni pamoja na, yaani
kukosha mikono pamoja na vifundo vya mikono. Hivi inathibiti kwa qauli ya Jabir
r.a. kuwa amemuona Mtume wetu Mpenzi s.a.w. anazungushia maji juu ya vifundo
vyake vya mikono. (Imepokewa na Darqu’tni na Al Baihaqy).
Na katika Hadithi yao
walioipokea kutoka kwa Jabir vilevile kuwa Mtume wetu Mpenzi s.a.w.
alizungushia maji juu ya vifundo vyake vya mikono na akasema:
Na ni lazima ili kutimia udhu
kufikisha maji katika unywele na ngozi ya kiungo cha udhu. Ikiwa kwenye kucha
kuna uchafu au juu ya ngozi kuna kitu kinachozuia maji kufika juu ya ngozi,
kama vile lami, mafuta, utomvu, basi udhu hausihi, kwa hivyo Sala yake haisihi.
Ya
Nne, kupaka maji kichwani (sehemu ya kichwa); kulingana na Qauli ya
Mwenyezi Mungu Mtukufu: “. … na mpake vichwa vyenu…” (Al Maaida :
6).
Kupaka maji kichwani huwa kwa
maji mengi au kidogo, hivi ni kutokana na Hadithi ya Al Mughaira r.a. kwamba:
“Mtume wetu Mpenzi s.a.w. ametia udhu na akapaka maji sehemu ya juu ya kipaji
cha uso na juu ya kilemba chake na juu ya khufaini*”. (Imepokewa na Muslim).
Lau kama ni fardhi kupaka maji
kichwa chote, basi Mtume wetu Mpenzi .s.a.w. asingalipaka maji juu ya sehemu ya
kipaji cha uso tu (juu ya nywele).
Ya
Tano, kuwosha miguu miwili pamoja na vifundo vyake; kulingana na
Qauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu: …na osheni miguu yenu mpaka
vifundo…". (Al Maida : 6).
Ya
Sita, kufululiza na kufuatiza; haya yamethibitika kutokana na hii
Aya iliofunza juu ya udhu - Al Maida : 6, kwani “wau”
, yaani "na" iliomo
kwenye Aya hii ni yenye kueleza juu ya mpangilizio. Pia haikupokewa kuwa Mtume
wetu Mpenzi s.a.w. amewahi kutia udhu bila ya mpangilizio kama ulivyokuja
kwenye Aya hii.
Vilevile Mtume wetu mpenzi
s.a.w. alisema baada ya kukamilisha kutia udhu maneno yenye maana kama hivi: “Huu
ndio udhu, hakubali Mwenyezi Mungu Mtukufu Sala ila kwa udhu kama huu”.
(Imehadithiwa na Al Bukhari).
Hadithi hii imetangulia
kutajwa hapo juu.
Vilevile ameeleza Mtume wetu
Mpenzi s.a.w.:
“Anzieni kwa alivyoanzia Mwenyezi Mungu
Mtukufu”. (Imehadithiwa na Al Nissaai).
Sunna za Udhu
Sunna za udhu ni kumi na moja:
Ya
Kwanza, kusomaa Bismillahi
wakati wa kuanza kutia udhu; haya ni kwa
yaliopokewa na Al Baihaqy r.a. kwamba Mtume wetu Mpenzi s.a.w. alitia mkono
wake kwenye chombo chenye maji na akawaambia Masahaba zake r.a.:
“Tieni udhu kwa Bismillahi.
Na kwa Hadithi ya Mtume wetu
Mpenzi s.a.w.:
Ya
Pili, kuosha viganja viwili vya mikono kabla ya kuvichovya kwenye
chombo chenye maji ya kutilia udhu, hivi ndivyo ilivyopokewa kuwa hivi ndivyo
namna ya kutia udhu Mtume wetu Mpenzi s.a.w. Vilevile ndivyo ilivyopokewa
kutoka kwa Ausi bin Ausi Al Thaqafi:
Vilevile imepokewa kutoka kwa
Sayyidna Othaman r.a. kuwa kasema:
Na haya yamethibiti kutokana
na Masahaba mbali mbali r.a.
Ya
Tatu Na Nne, kusukutua na kuvutia maji puwani; hivi ni kama
ilivyoonekana akifanya Mtume wetu Mpenzi s.a.w., na kwa qauli yake Mtume wetu
Mpenzi s.a.w. yenye maneno na maana kama hivi:
(mambo) kumi ni katika suna”, ikahisabiwa
miongoni mwa kumi hayo ni kusukutuwa na kuvutia maji puwani. (Imepokewa na
Muslim).
Kutanguliza kusukutuwa kabla
ya kuvutia maji puwani ni sharti ya kupatikana suna hii. Inapendekezwa kufanya
mno hivi kwa asiekuwa kafunga, ama aliefunga ni karaha kwake kufanya hivi,
(kuogopewa yasimponyoke maji yakaingia tumboni, akafungua).
Ya
Tano, kupaka maji kichwa chote; hivi ni kama ilivyoonekana akifanya
Mtume wetu Mpenzi s.a.w., na pia kuepukana na tafauti za rai. Na ni suna kuanza
kwenye kipaji cha uso na kuipeleka mikono miwili mpaka mwisho wa kichwa na
kuirejesha mpaka ulipoanzia. Imepokewa hivi kutoka kwa Abdulla bin Zaid r.a.
akieleza namna ya kutia udhu kwa Mtume wetu Mpenzi s.a.w. (Imehadithiwa na
Jamaa wapokeaji Hadithi).
Ya
Sita, kuosha masikio nje na ndani kwa maji mepya. Ameeleza Bwana
Abdulla bin Zaid r.a. kuwa amemuona Mtume wetu Mpenzi s.a.w. akitia udhu,
akachukuwa maji mepya mbali na yale aliopangusia kichwa akaoshea masiakio.
(Imehadithiwa na Al Hakim na Al Baihaqy).
Hufanya hivi kuosha masikio
kwa kutia maji mepya mikononi kisha kutia vidole vya shahada masikioni na
vidole vya gumba nje ya masikio na kuvizungusha polepole.
Ya
Saba, kuesua (kupapachua) ndevu nyingi, (ndevu nyingi ni zile ambazo
ngozi ya kidevu haionekani). Haya kama ilivyopokewa kutoka kwa Ibni 'Abbas r.a.
ya kwamba Mtume wetu Mpenzi s.a.w. alikuwa anapotia udhu hupapachua ndevu zake
kwa vidole vyake. (Imehadithiwa na Ibnu Majah).
Na imepokewa kutoka kwa Ibni
'Abbas vilevile kuwa: “Mtume wetu Mpenzi s.a.w. alikuwa akipapachua ndevu
zake”.
Amesema Al Bukhari: “Hivi ni
sahihi zaidi ilivyo kwenye mlango wa udhu na Hadithi ya Ibni 'Abbas r.a. kuwa
Mtume wetu Mpenzi s.a.w. alikuwa anapotia udhu hupapachua ndevu zake kwa vidole
vyake kwa kuanzia chini ya kidevu. (Imehadithiwa na Ibnu Maajah).
Ya
Nane, kuesua (kupapachua) vidole vya viganja pamoja na vidole vya
miguu. Haya ni kutokana na Hadithi ya Mtume wetu Mpenzi s.a.w.:
Kuesua (kupapachua) vidole vya
miguu ni kwa kupitisha kidole kidogo cha mkono wa kushoto kwa kuanzia chini ya
kidole kidogo cha mguu wa kulia na kumalizia kidole kidogo cha mguu wa kushoto.
Ama kupapachua vidole vya viganja ni kwa kupitisha baina ya vidole.
Ya
Tisa, kutanguliza kulia kabla ya kushoto. Haya ni kwa Hadithi ya
Mtume wetu mpenzi s.a.w.:
“Mkitia udhu anzieni kwa vya kuliani vyenu”.
(Imehadithiwa na Abu Daud na Ibnu Maajah, na Ibnu Khuzaimah na Ibnu Hibban
wameipa darja ya Hadithi sahihi).
Ya
Kumi, kuosha mara tatu tatu; hivi ni kwa Hadith ya Sayyidna Othman
r.a. kwamba Mtume wetu Mpenzi s.a.w. akitia udhu kwa kuosha mara tatu tatu.
(Imepokelewa na Muslim). Na kwa ilivyopokewa na Abu Daud r.a. kutoka kwa
Sayyidna Othman r.a. ya kwamba Mtume wetu Mpenzi s.a.w. amepangusa kichwa chake
mara tatu. Na ilivyosimuliwa na Ibn Maajah r.a. kwamba Sayyidna 'Ali r.a.
ametia udhu kwa kuosha mara tatu tatu; na akasema Sayyidna 'Ali r.a.: "Huu
ndio udhu wa Mtume s.a.w.".
Kumi
na Moja, kufululiza na kufuatiza; hivi ni kama alivyofanya Mtume
wetu Mpenzi s.a.w. na kufanya hivi ni kuepukana na khilafu za wanazuoni.
Inapendekezwa ukikamilisha kutia udhu asikunute wala usifute mikono yako, hivi
ni kutokana na Hadith ya Mtume wetu Mpenzi s.a.w.:
Kwani hivi kukunuta mikono
baada ya kukamilisha kutia udhu huwa ni kama kujikunuta kutokana na hii ibada
ya kutia udhu. Na inapendekezwa aongeze baada ya Bismillah kwa kusema:
Na aizungushe pete ikiwa maji
yanafika chini ya hio pete aliovaa, ikiwa hayafiki maji chini ya pete inapasa
aivue ili maji yaweze kufika chini ya pete. Anapotia udhu, akikosha uso aanzie
kwa kukosha sehemu ya juu ya uso na ya kichwa, yaani kwenye kipaji cha uso; na
wakati wa kukosha mikono na miguu aanzie kwenye ncha za vidole ikiwa anajitilia
maji mwenyewe. Akiwa anatiliwa maji, na mtu, au anatia udhu kwa mfereji, aanzie
kwenye vifundo, vya mikono au vya miguu.
Imependekezwa maji ya kutilia
udhu yasipungue kibaba, wala asifanye israfu ya maji, wala asizidishe mara tatu
tatu, wala asizungumze wakati anapotia udhu, wala asipige uso wake kwa maji. Na
kama ilivyopokewa na Muslim kuwa akikamilisha kutia udhu asome du'a hii:
Akaongeza alivyopokea Al
Tirmidhy r.a.:
Na akaongeza alivyopokea Al
Haakim:
Vile vile inasuniwa baada ya kukamilisha
kutia udhu kusali rakaá mbili za sunna, hivi ni kutokana na Hadithi ya
Mtume wetu Mpenzi s.a.w.:
"Hatii udhu mmoja
wenu na akafanya vyema katika kutia udhu wake na akasali raka'a mbili za suna,
akielekea kwa moyo wake na kwa uso wake, isipokuwa huwajibikia juu yake
Pepo". (Imehadithiwa na Muslim).
Na tambua na ufahamu, lau
akitia shaka wakati anatia udhu kuwa amekikosha kiungo maalumu cha udhu, au
hakukikosha, haihisabiwi, kwani asili yake ni kuwa hakikukoshwa, yaani
huchukuliwa kuwa hakukikosha. Ama akitia shaka baada ya kukamilisha kutia udhu,
basi haichukuliwi hio shaka; hivyo ni kwa sababu lenye kutarajiwa ni kukamilia
hivyo kutia udhu kwake, na kwa vile kuyumkinika kuendelea hio shaka.
Post a Comment