Khushuu YA Ajabu Katika Swalah
Ni
mtoto wa Asmaa bint Abubakar ambaye pia ni dada yake bibi 'Aishah mke
wa Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Baba yake ni
Zubayr ambaye ndiye mume wa Asmaa bint Abubakar (Radhiya Allahu 'anha).
Alipatwa
na maradhi ya saratani (cancer) katika mguu wake, akaambiwa na
madaktari kuwa lazima akatwe mguu wake ili maradhi yasienee mwilini
mwake. Kwa hivyo hana budi ila anywe pombe ili asihisi maumivu. (Zama
hizo kulikuwa hakuna sindano au dawa za kisasa za kuondosha fahamu ya
mtu anapofanyiwa operesheni). Alipoambiwa hivyo 'Urwah alijibu: "Moyo
wangu na ulimi wangu upotee katika kumkumbuka Allaah? WaLlahi sitoingia
katika maasi kwa ajili hiyo". Wakamwambia: "Tutakupa kileweshacho
(kuondosha fahamu) kama vile unusukaputi". Akasema: "Sipendi kuchomolewa
kipande katika mwili wangu nikiwa katika hali ya kulala". Wakamwambia:
"Tumlete mtu akukamate". Akasema: "Niachilieni mwenyewe hivi hivi"
(yaani mnikate huu mguu hivi hivi bila ya kunipa chochote). Wakamwambia:
"Hutoweza kuvumilia". Akasema: "Niacheni niswali. Mtakakaponiona
sitingishiki nikiwa nimetuliza misuli yangu nikiwa niko imara nisubirini
hadi nitakapokwenda kusujudu. Kisha nitakaposujudu hapo huwa sifikirii
dunia. (Maana kwamba huwa sioni wala sisikii lolote, wa kuhisi chochote
wala sina habari ya lolote isipokuwa niko na Mola wangu katika khushuu).
Hapo tena fanyeni mnavyotaka kunifanya".
Akaja daktari akasubiri. Aliposujudu 'Urwah, daktari akaleta msumeno akamkata mguu wake. Hakuwa anasema kitu 'Urwah isipokuwa:
لا إلهَ إلاّ اللّه, رَضيـتُ بِاللهِ رَبَّـاً وَبِالإسْلامِ ديـناً وَبِمُحَـمَّدٍ صََلى الله عليه وسلم نَبِيّـاً وَرَسُولاً .
Laa Ilaa Illah Allaah, Radhwiytu BiLlaahi Rabba, wa bil-Islaami Diyna, wa bi Muhammadin Swalla Allahu 'alayhi wa wa aalihi wa sallam Nabiyyaw-wa Rasuula".
“Nimeridhika
kuwa Allaah Ndiye Mola wangu, na Uislamu ndio dini yangu, na Muhammad
Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam kuwa ni Mtume na Mjumbe
wangu”.
Akaendelea
hivyo hadi akamaliza daktari kazi yake ya kumkata mguu, damu ikiwa
inamchirizika. Hakupiga kelele 'Urwah wala kuugua kwa maumivu!
Alipozindukana
'Urwah, akaletewa mguu wake akautazama, huku akiuambia: "Naapa kwa
Allaah! Sijapata kukupeleka (kutembea nao mguu huu) katika mambo ya
haram, na Allaah Anajua. Mara ngapi nimesimama nawe usiku kwa ajili ya
Allaah!". Mmoja wao akamuambia: "Ee 'Urwah! Bishara! (Au pongezi!)
Kipande cha mwili wako kimetangulia Peponi!". Akasema: WaLlahi hajapata
mtu kuniliwaza maliwazo bora kama haya!
Post a Comment