Nini Khuffu mbili? 
Khaufi ni mfano wa soksi ambazo
huvaliwa bila ya viatu na huweza kwendea masafa kwa miguu. Aghlabu hufanywa
kutokana na ngozi ya wanyama-howa, kama vile kondoo, mbuzi au ngamia. Matumizi
yake aghalabu ni kuvaliwa katika safari za jangwani.
Kujuzu Kupangusa Juu Ya Khuffu Mbili
Inajuzu kupangusa juu ya khuffu
mbili kwa alioyapokea Imam Muslim r.a. kutoka kwa Jarir r.a. aliesema kuwa:
Shuruti za Kujuzu Kupangusa Juu ya Khuffu mbili
Kujuzu kupangusa juu ya khuffu
mbili kuna shuruti mbili:
Kwanza, iwe
khuffu mbili zote mbili zimevaliwa hali ya kuwa ana 'tahara kaamili. Lau kama
ataosha mguu mmoja kisha akavaa khaufa moja, kisha akaosha mguu wa pili na
akavaa khaufa ya pili; haitajuzu kupangusa juu ya khuffu mbili hizo. Hivi ni
kutokana na Hadithi ya Al Mughaira r.a. aliposema kuwa alimtilia maji Mtume
wetu Mpenzi s.a.w. kwa kutia udhu, alipofika kukosha miguu alitaka kuzivua
khuffu mbili zake; Mtume wetu Mpenzi s.a.w. akamwambia asizivue kwa qauli yake
s.a.w.:
Na ameeleza Imam Shafi'ii r.a.
kutoka kwa Al Mughaira ya kwamba alisema: "Nikasema: "Ewe Mtume wa
Mwenyezi Mungu nipanguse juu ya khuffu mbili"? Akasema Mtume wetu Mpenzi
s.a.w.:
"Naam,
ikiwa utazivaa na miguu yako ni 'taahir".
Pili, iwe hizo
khuffu mbili zinafaa kupangusika. Ili kufaa kupangusa juu ya khuffu mbili kuna
mambo kadhaa.
La Kwanza, iwe hizo
khuffu mbili zinafunika sehemu yote ya mguu yenye kulazim katika kutia udhu.
Ikiwa sehemu yoyote ya mguu yenye kulazim katika kutia udhu haikufunikika kwa
hio/hizo khuffu mbili basi haitajuzu kupangusa juu ya khaufani. Hivi kwa sababu
ile sehemu ambayo haikufunikika kwa khuffu mbili - moja au zote mbili - itakuwa
inalazim kuoshwa kwa kutia udhu, na ile sehemu iliofunikika itakuwa waajibu ni
kupanguswa. Kwa vile hakuna hukmu ya kukosha na kupangusa wakati mmoja, itabidi
kukosha miguu yote miwili kwa kutia udhu kaamil, kwani kukosha ndio asili
katika kutia udhu.
La Pili, iwe hizo
khuffu mbili madhubuti za kumuwezesha msafiri kuziendea kwa mujib wa haja yake,
tangu kuondoka kwake mpaka kurejea kutoka safari yake; kwa sababu hii ruhusa ya
kupangusa juu ya khufaini ni kwa ajili ya haja ya kuzivaa na kumuwezesha
kuziendea. Na uchache wa masafa yenye kukubalika umadhubuti wa khuffu mbili ni
kuweza kuendewa si chini ya meli tatu, hivi ndivyo alivyosema Imam Al Ghazali
r.a., na amekadiria Sheikh Abu Muhamed kwa masafa yenye kuruhusiwa Sala ya
safari; hivi ndivyo ilivyokubaliwa na kutegemewa na Maimam wengi. Ama ikiwa
hizo khuffu mbili hazifai kutumika kwa kwendea kama hivi ilivyoelezwa hapa, ima
kwa kuwa si madhubuti, kama vile kuwa zimefanywa kwa kitambaa; kama vile soksi
ambazo hazizuii kuingia maji, au kwa ugumu wake, kama vile kuwa zimefanywa kwa
chuma au kitu cha mfano wa chuma; katika hali hizi haitajuzu hukmu ya kupangusa
juu yake.
La Tatu, ziwe
zinazuia kuingia maji; ikiwa hazizuii kuingia maji basi haitajuzu hukmu ya
kupangusa juu yake; hivi ndivyo walivyokubaliana Maimam wengi.
La Nne, ziwe hizo
khuffu mbili ni 'taahir, kwani Sala haisihi kwenye najsi; kwa hivyo haitajuzu
hukmu ya kupangusa ikiwa hizo khuffu mbili si 'taahir, kwa kupatwa na najsi au
kwa kuwa zimefanywa kutokana na kitu ambacho ni najsi.
Muda wa Kuendelea Kujuzu Kupangusa
Mtu aliokuwa hayumo safarini
anaruhisiwa kupangusa juu ya khuffu mbili muda wa siku moja (mchana na usiku
wake), yaani saa 24. Kwa aliemo safarini anaruhusiwa kupangusa juu ya khuffu
mbili muda wa siku (mchana na usiku wake) tatu, yaani saa 72. Hivi ni kutokana
na Hadithi ya Sayyidna Abu Bakar r.a. kwamba Mtume wetu Mpenzi s.a.w.:
Na kutoka kwa 'Safwani bin 'Assal
r.a. kuwa kasema:
"Alikuwa Mtume wetu Mpenzi
s.a.w. tukiwa kwenye safari anatuamrisha tusivue khaufi zetu kwa muda wa siku
tatu, isipokuwa kwa kupatwa na janaba; lakini kwa haja ndogo au haja kubwa au
kwa kulala tusivue". (Imehadithiwa na Al Nissaai na Al Tirmidhy).
Haya yote imeshurutishwa ya kwamba
safari yenyewe isiwe katika maasi, ikiwa si hivyo, yaani ikiwa safari ya katika
maasi; basi ataruhusiwa kupangusa kwa hukmu ya muqim (asiekuwa msafirini),
yaani siku moja.
Kuanza Muda wa Kupangusa
Unaanza muda wa kupangusa tangu
pale kupatwa na hadathi - ndogo au kubwa - baada ya kuzivaa hizo khuffu mbili,
sio tangu pale kuzivaa hizo khufaini, hivi ni kwa sababu huku kupangusa juu ya
khufaini ni ibada ya wakati maalum (kama vile ilivyo Sala), na wakati wake ni
pale inapojuzu kufanya hivyo, yaani kupangusa. Na amesema mwanazuoni, Daud Al
Dhaahiry r.a. kwamba muda unaanza tangu pale kuzivaa hizo khuffu mbili, sio
tangu pale kupatwa na hadathi.
Imam Al Nawawy r.a. yeye amesema
kuwa ni kuchagua baina ya rai mbili hizi zilizotajwa hapo juu, hivi ni kwa vile
kuwa Hadithi zote zilizokuja juu ya suala hili ni sahihi; na rai mbili hizi
zimejengeka juu ya Hadithi hizo za Mtume wetu Mpenzi s.a.w. Ikiwa atapangusa
juu ya khuffu mbili wakati ni msafiri, kisha akawa muqim, au akapangusa wakati
ni muqim, kisha akasafiri; atatimiza kwa muda wa muqim. Hivi ni kwa vile
kukusanyika hali mbili, yaani hali ya kuwa ni msafiri na hali ya kuwa ni muqim;
basi hukmu ya muqim ndio yenye kutumika, kwa vile kuwa ndio asli ya hukmu.
Hivi ni sawa lau kuwa kaanza Sala
zake wakati ni muqim, kisha akasafiri, basi haitajuzu kwake kusali safari
(kupunguza Sala) zile Sala ambazo ilikuwa azisali wakati ni muqim; hivi ni kwa
sababu hukmu ya muqim ndio asli ya hukmu. Ikiwa msafiri atatia shaka kuwa
ameanza kupangusa juu ya khuffu mbili hali ya kuwa ni muqim au msafari; basi atachukuwa
hukmu ya muqim, kwani ndio asli ya hukmu.
Namna ya Kupangusa Juu ya Khuffu Mbili
Uchache wa kupangusa juu ya khuffu
mbili ni vile kupangusa kunakojuulika kwa dasturi kuwa ni kupangusa, na huwa
kwa kuanzia sehemu ya juu ya kila ya moja ya hizo khuffu mbili. Hivi ni
kutokana na Hadithi ya Al Mughaira r.a. alivyosema:
Na ukamilifu wa kupangusa ni
kupangusa juu ya hizo khuffu mbili na chini yake, hivi ni kutokana na Hadithi
ya Al Mughaira bin Sha'abat r.a.:
Kupangusa huwa kwa kuweka mkono wa
kushoto chini ya sehemu ya kisigino na mkono wa kulia juu ya sehemu ya vidole,
kisha aupitishe mkono wa kulia mpaka mwisho wa sehemu ya kisigino na mkono wa
kushoto aupitishe mpaka sehemu ya juu ya vidole vyake huku amechawanya vidole
vyake vya mkono.
Yenye Kutenguwa Kupangusa Juu ya Khuffu Mbili
Inatenguka kupangusa juu ya khuffu
mbili kwa mambo matatu:
La Kwanza, kuivua
moja ya khuffu mbili au zote mbili, au zikawa khuffu mbili au moja yao haifai
tena kutumika, ama kwa kutoboka, au kuwa dhaifu. Katika hali hii itamlazim
kukosha miguu tu, ikiwa bado anao udhu, ikiwa atakuwa hana udhu basi itamlazim
atie udhu kaamili.
La Pili, kumalizika
muda ulio ruhusiwa kupangusa, yaani kwa msafiri ikipita siku tatu; na kwa muqim
siku moja. Ukimalizika muda itabidi atie udhu na kuzivaa upya.
La Tatu, ikimlazim
kukoga. Vilevile ikiwa mguu wake utaingia najsi na ikawa hawezi kuindoa hio
najsi mpaka kwa kuivua khauf yake, itamlazim aivue na kwa hivyo itaba'tilika
kufaa utumizi wa khuffu mbili. Ama ikiwa ataweza kuinadhifisha hio khauf
kutokana na najsi bila ya kuivua, atafanya hivyo na itaendelea kujuzu utumiaji
wa khuffu mbili kwa muda wake.
Post a Comment