Hukmu Ya Muziki Katika Qur-aan Na Sunnah
Ewe Upendaye Nyimbo Na Muziki, Haujafika Wakati Wa Kuogopa Adhabu Kali Za Allaah?
Muziki ni haraam kutokana na dalili dhahiri tulizopewa katika Qur-aan na Hadiyth za Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam).
Baadhi ya watu katika Jamii yetu bado hawajatambua uharamu wa jambo
hili, tunasikia wengi bado wanaimba taarabu au miziki mbalimbali, na
mara kwa mara unapomnasihi nduguyo Muislamu kuacha maasi haya, jibu mara
nyingi huwa: "Tena nyinyi mmezidi! Wapi inasema kuwa nyimbo haramu" Au
wengine waliobobea katika maradhi haya hunena: "Mimi yote naweza kuacha
lakini nyimbo utaniua", husema hivyo bila ya kujali amri ya makatazo ya
Mola Mtukufu ambaye ni Muweza wa kuyaua masikio yake awe kiziwi na
asiweze kusikia tena hizo nyimbo.
Inafika hadi Muislam hawezi kulala
hadi alazwe kwa muziki, hawezi kula ila muziki uwe unapigwa, hawezi
kufanya kazi za nyumbani bila muziki kufunguliwa, hawezi mtu kutembea
bila kuwa na walkman au mp3 yake ikicheza muziki, hawezi kufanya kazi akiwa
kazini…hawezi kusafiri…hawezi hata kufanya mazoezi ya ndani bila kuwepo
na muziki wa kumchochea na kumtia hamasa (kama wanavyoitakidi) ya lile
analolifanya kwa wakati huo! ‘Alaa kulli haal, muziki umekuwa ni sehemu
kiungo kikubwa cha maisha ya mwanaadam kwa wakati huu!
Hivyo tumeona
kuna umuhimu mkubwa wa kuwakumbusha ndugu zetu waepukane na haramu hii
ili wajiokoe na ghadabu za Mola Mtukufu, ghadhabu kali ambazo zinafika
kumgeuza mtu awe nyani au nguruwe kama tutakavyosoma katika hizi dalili
za wazi wazi zenye uhakika.
Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) katika suuratu Luqmaan:
(( ﻭَﻣِﻦَ ﺍﻟﻨَّﺎﺱِ ﻣَﻦ ﻳَﺸْﺘَﺮِﻱ ﻟَﻬْﻮَ ﺍﻟْﺤَﺪِﻳﺚِ ﻟِﻴُﻀِﻞَّ ﻋَﻦ
ﺳَﺒِﻴﻞِ ﺍﻟﻠَّﻪِ ﺑِﻐَﻴْﺮِ ﻋِﻠْﻢٍ ﻭَﻳَﺘَّﺨِﺬَﻫَﺎ ﻫُﺰُﻭًﺍ ﺃُﻭﻟَﺌِﻚَ ﻟَﻬُﻢْ
ﻋَﺬَﺍﺏٌ ﻣُّﻬِﻴﻦٌ ))
((Na miongoni mwa watu wapo wanaonunua maneno
ya upuuzi, ili wawapoteze watu na njia ya Mwenyezi Mungu pasipo kujua,
na wanaichukulia ni maskhara. Hao watapata adhabu ya kuwafedhehesha))
[Luqmaan: 6]
Ibn Mas'uud (Radhiya Allaahu 'anhu) amesema kuhusu
Aayah hii "Naapa kwa Allaah hii inamaanisha ni kuimba (nyimbo na
miziki)" [At-Twabariy 20:127]
ﻭﻋﻦ ﺍﺑﻦ ﻋﺒﺎﺱ ﻗﺎﻝ ﻋﻦ ﺁﻳﺔ : )) ﻭﻣﻦ ﺍﻟﻨﺎﺱ ﻣﻦ ﻳﺸﺘﺮﻱ ﻟﻬﻮ ﺍﻟﺤﺪﻳﺚ (( ، ﻗﺎﻝ : ﺍﻟﻐﻨﺎﺀ ﻭﺃﺷﺒﺎﻫﻪ ﺇﺳﻨﺎﺩﻩ ﺻﺤﻴﺢ - ﺍﻟﻤﺤﺪﺙ : ﺍﻷﻟﺒﺎﻧﻲ
Na Ibn 'Abbaas (Radhiya Allaahu 'anhuma) pia amesema kuhusu Aayah hii : ((Na miongoni mwa watu wapo wanaonunua maneno ya upuuzi)) "Ni nyimbo
na maneno ya yanayofanana (ya upuuzi)" [Isnaad Sahiyh kutoka kwa Shaykh
Al-Albaaniy]
GHADHABU ZA ALLAAH KUWAANGAMIZA WAFANYAO MAASI HAYA (YA KUSIKILIZA NYIMBO NA MIZIKI
Vile vile ghadhabu za Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) ni kali mno za kuangamizwa pindi maasi haya yatakapodhihirika.
ﻋﻦ ﻋﻤﺮ ﺑﻦ ﺣﺼﻴﻞ ﻋﻦ ﺭﺳﻮﻝ ﺍﻟﻠﻪ ﺻﻠﻰ ﺍﻟﻠﻪ ﻋﻠﻴﻪ ﻭﺳﻠﻢ ﺍﻧﻪ ﻗﺎﻝ : )) ﻳﻜﻮﻥ ﻓﻰ
ﺍﻣﺘﻰ ﻗﺬﻑ ﻭﻣﺴﺦ ﻭﺧﺴﻒ :(( ﻗﻴﻞ ﻳﺎﺭﺳﻮﻝ ﺍﻟﻠﻪ ﻭﻣﺘﻰ ﺫﻟﻚ ﻗﺎﻝ : )) ﺍﺫﺍ ﻇﻬﺮﺕ
ﺍﻟﻤﻌﺎﺯﻑ … (( ﺍﺧﺮﺟﻪ ﺍﻟﺘﺮﻣﺬﻯ ﻭﺻﺤﺤﻪ ﺍﻟﻌﻼﻣﻪ ﺍﻻﻟﺒﺎﻧﻰ
Mtume (Swalla
Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kasema: ((Kutatokea katika Ummah
huu maafa ya kuteremshiwa mawe kutoka mbinguni, kugeuzwa maumbile ya
binaadamu [kugeuzwa kufanywa nyani na nguruwe] na mididimizo [ya ardhi].
Ikaulizwa: Ewe Mjumbe wa Allaah, lini yatatokea hayo? Akasema:
((Itakapodhihirika miziki … ))
[At-Trimidhy na ameipa daraja ya Sahiyh Shaykh Al-Albaaniy]
TUSIKILIZE NA KUSOMA QUR-AAN
Muziki na nyimbo humjaza mtu mapenzi makubwa moyoni, zimshughulishe
zaidi hadi asiwe na muda wa kusoma maneno ya Mola wake Mtukufu ambayo
hiyo ndio inayopasa kuifanya iwe midomoni na moyoni mwetu daima kwa
kusoma kwa sauti nzuri ya kupendeza (Tajwiyd) kama tulivyoamrishwa na
Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam).
SAUTI ZA NYIMBO (NA MIZIKI) ZIMELAANIWA DUNIANI NA AKHERA
ﻗﺎﻝ ﺭﺳﻮﻝ ﺍﻟﻠﻪ ﺻﻠﻰ ﺍﻟﻠﻪ ﻋﻠﻴﻪ ﻭﺳﻠﻢ : )) ﺻﻮﺗﺎﻥ ﻣﻠﻌﻮﻧﺎﻥ ﻓﻰ ﺍﻟﺪﻧﻴﺎ ﻭﺍﻻﺧﺮﻩ
ﻣﺰﻣﺎﺭ ﻋﻨﺪ ﻧﻌﻤﻪ ﻭﺭﻧﻪ ﻋﻨﺪ ﻣﺼﻴﺒﻪ )) ﺍﻟﺒﺰﺍﺭ ﻭ ﺻﺤﺤﻪ ﺍﻟﻌﻼﻣﻪ ﺍﻻﻟﺒﺎﻧﻰ
Na
kasema Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): ((Sauti
mbili maluuni [zilizolaaniwa] duniani na Akhera; mizumari katika furaha
na kuombeleza katika misiba)) [Al-Baazaar – na Shaykh Al-Albaaniy kaipa
daraja ya Sahiyh]
NI SUNNAH KUZIBA MASIKIO UNAPOSIKIA MUZIKI BILA YA KUTAKA
ﻋﻦ ﻧﺎﻓﻊ ﺃﻧﻪ ﻗﺎﻝ : ﺳﻤﻊ ﺍﺑﻦ ﻋﻤﺮ ﻣﺰﻣﺎﺭﺍ، ﻗﺎﻝ : ﻓﻮﺿﻊ ﺃﺻﺒﻌﻴﻪ ﻋﻠﻰ ﺃﺫﻧﻴﻪ، ﻭﻧﺄﻯ
ﻋﻦ ﺍﻟﻄﺮﻳﻖ، ﻭﻗﺎﻝ ﻟﻲ : ﻳﺎ ﻧﺎﻓﻊ ﻫﻞ ﺗﺴﻤﻊ ﺷﻴﺌﺎ؟ ﻗﺎﻝ : ﻓﻘﻠﺖ : ﻻ ! ﻗﺎﻝ : ﻓﺮﻓﻊ
ﺃﺻﺒﻌﻴﻪ ﻣﻦ ﺃﺫﻧﻴﻪ، ﻭﻗﺎﻝ : ﻛﻨﺖ ﻣﻊ ﺍﻟﻨﺒﻲ ﺻﻠﻰ ﺍﻟﻠﻪ ﻋﻠﻴﻪ ﻭﺳﻠﻢ، ﻓﺴﻤﻊ ﻣﺜﻞ ﻫﺬﺍ !
ﻓﺼﻨﻊ ﻣﺜﻞ ﻫﺬﺍ - ﺣﺪﻳﺚ ﺻﺤﻴﺢ، ﺻﺤﻴﺢ ﺃﺑﻲ ﺩﺍﻭﻭﺩ ﻭﺭﺍﺟﻊ ﺍﻟﺴﻠﺴﻠﺔ ﺍﻟﺼﺤﻴﺤﺔ ﻟﻸﻟﺒﺎﻧﻲ
Kutoka kwa Naafi'i ambaye amesema, amesikia sauti ya muziki akaziba
masikio yake kwa vidole vyake, kisha akamgeuza mnyama wake aliyempanda
[arudi asiendelee kwenda sehemu hiyo iliyokuwa na muziki] akasema: "Ewe
Naafi'i, umesikia kitu?" Akasema, nikajibu: "Hapana". Akaondosha vidole
vyake masikioni mwake akasema: "[siku moja] Nilikuwa na Mtume (Swalla
Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliposikia kama hivi [muziki]
akafanya kama hivi [nilivyofanya mimi yaani kuziba masikio yake asisikie
sauti ya mizumari] [Hadityh Swahiyh ya Abu Daawuud na Ikiwa katika
Silsilatus-Swahiyha ya Shaykh Al-Albaaniy]
ﻭﻗﺎﻝ ﺭﺳﻮﻝ ﺍﻟﻠﻪ ﺻﻠﻰ ﺍﻟﻠﻪ
ﻋﻠﻴﻪ ﻭﺳﻠﻢ : )) ﻟﻴﻜﻮﻧﻦ ﻣﻦ ﺃﻣﺘﻲ ﺃﻗﻮﺍﻡ ﻳﺴﺘﺤﻠﻮﻥ ﺍﻟﺤﺮ ﻭ ﺍﻟﺤﺮﻳﺮ ﻭ ﺍﻟﺨﻤﺮ ﻭ
ﺍﻟﻤﻌﺎﺯﻑ، ﻭ ﻟﻴﻨﺰﻟﻦ ﺃﻗﻮﺍﻡ ﺇﻟﻰ ﺟﻨﺐ ﻋﻠﻢ، ﻳﺮﻭﺡ ﻋﻠﻴﻬﻢ ﺑﺴﺎﺭﺣﺔ ﻟﻬﻢ، ﻳﺄﺗﻴﻬﻢ
ﻟﺤﺎﺟﺔ، ﻓﻴﻘﻮﻟﻮﻥ : ﺍﺭﺟﻊ ﺇﻟﻴﻨﺎ ﻏﺪﺍ، ﻓﻴﺒﻴﺘﻬﻢ ﺍﻟﻠﻪ، ﻭﻳﻀﻊ ﺍﻟﻌﻠﻢ، ﻭﻳﻤﺴﺦ ﺁﺧﺮﻳﻦ
ﻗﺮﺩﺓ ﻭﺧﻨﺎﺯﻳﺮ ﺇﻟﻰ ﻳﻮﻡ ﺍﻟﻘﻴﺎﻣﺔ )) ﺭﻭﺍﻩ ﺍﻟﺒﺨﺎﺭﻱ
Na akasema Mtume
(Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): ((Watakuweko watu katika
Ummah wangu watakaojaribu kuhalilisha zinaa, uvaaji wa hariri, pombe na
muziki. Baadhi ya watu watakuwa pembeni mwa mlima na mchungaji wao
atawajia jioni na kuwaomba haja [fulani]. Watasema: "Rudi kesho". Allaah
Atawaangamiza usiku, Atawaangushia milima kisha Atawabadilisha
waliobakia wawe nyani na nguruwe na watabakia hivyo hadi siku ya
Qiyaamah))[Al-Bukhaariy]
Hadiyth hii inatuthibitishia kuwa madhambi
yote hayo yako sawa sawa uharamu wake, kama vile zinaa na pombe ilivyo
haramu, basi na muziki pia haramu sawa sawa. Sasa vipi Muislamu aone
kuwa muziki sio maasi makubwa ya kujiepusha nayo?
Imaam Abu Haniyfah
amesema: "Kuimba (nyimbo, ngoma) ni katika madhambi makubwa ambayo
inatakiwa Muislamu kujiepusha nayo haraka"
Khofu zaidi imuingie
Muislamu kuwa anaweza kupata adhabu ya kugeuzwa nyani au nguruwe kwa
maasi haya kama tulivyoonywa katika Hadiyth ifuatayo:
ﻭﻗﺎﻝ ﺭﺳﻮﻝ ﺍﻟﻠﻪ
ﺻﻠﻰ ﺍﻟﻠﻪ ﻋﻠﻴﻪ ﻭﺳﻠﻢ : )) ﻟﻴﺸﺮﺑﻦ ﺃﻗﻮﺍﻡ ﻣﻦ ﺃﻣﺘﻲ ﺍﻟﺨﻤﺮ ﻳﺴﻤﻮﻧﻬﺎ ﺑﻐﻴﺮ ﺍﺳﻤﻬﺎ
ﻳﻌﺰﻑ ﻋﻠﻰ ﺭﺅﻭﺳﻬﻢ ﺑﺎﻟﻤﻌﺎﺯﻑ ﻭﺍﻟﻤﻐﻨﻴﺎﺕ ، ﻳﺨﺴﻒ ﺍﻟﻠﻪ ﺑﻬﻢ ﺍﻷﺭﺽ ﻭﻳﺠﻌﻞ ﻣﻨﻬﻢ ﻗﺮﺩﺓ
ﻭﺧﻨﺎﺯﻳﺮ )) ﻗﺎﻝ ﺍﻟﺸﻴﺦ ﺍﻷﻟﺒﺎﻧﻲ - ﺭﺣﻤﻪ ﺍﻟﻠﻪ ﺗﻌﺎﻟﻰ - : ﺻﺤﻴﺢ
Na kasema
Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): ((Watu katika Ummah
wangu watakunywa pombe wakiipa jina jengine lisilokuwa hilo, miziki
itapigwa kwa ajili yao na watakuweko waimbaji wanawake. Allaah
Atawadidimiza ardhini na Atawageuza wawe nyani na nguruwe)) [Ibn Maajah
na Shaykh Al-Albaaniy ameipa daraja ya Sahiyh]
ﻧﺴﺄﻝ ﺍﻟﻠﻪ ﺍﻟﻌﺎﻓﻴﺔ ﻭﺍﻟﺴﻼﻣﺔ
Tunamuomba allaah azilainishe nyoyo zetu tuwe ni wenye kusikia na kutii
Meat Tarts With White Sauce
-
Ingredients:
Dough:
1½ cups flour
½ tsp salt
½ cup chilled butter pieces
4-5 Tbsp cold water
The filling:
Cooked minced meat (or chicken pieces), ...
Post a Comment