USAHIHI WA DU'AA YA KUFUTURU

Shaykh Yahyaa Al-Hajuwriy (Hafidhwahu Allaah)



SWALI:

Ni ipi hukmu ya Hadiyth hii:
ذَÙ‡َـبَ الظَّÙ…َـأُ، ÙˆَابْتَÙ„َّـتِ العُـروق، ÙˆَØ«َبَـتَ الأجْـرُ Ø¥ِÙ†ْ شـاءَ اللهُ
“Kiu kimeondoka na mishipa imelainika, na yamethibiti malipo Allaah Akipenda”

Je, kuna du’aa yoyote iliyothibiti ya kwa ajili ya kufungulia swawm?


JIBU:

Hiyo Hadiyth si sahihi.

Mwenye kufunga du’aa yake inaitikiwa, ikiwa ataomba wakati wa kufuturu au kabla ya kufuturu.

Allaah Anasema:
ÙˆَÙ‚َالَ رَبُّÙƒُÙ…ُ ادْعُونِÙŠ Ø£َسْتَجِبْ Ù„َÙƒُÙ…ْ ۚ Ø¥ِÙ†َّ الَّذِينَ ÙŠَسْتَÙƒْبِرُونَ عَÙ†ْ عِبَادَتِÙŠ سَÙŠَدْØ®ُÙ„ُونَ جَÙ‡َÙ†َّÙ…َ دَاخِرِينَ﴿٦٠﴾
60. Na Rabb wenu Amesema: “Niombeni, Nitakuitikieni. Hakika wale wanaotakabari na kuniabudu wataingika Jahanam wadhalilike. [Ghaafir: 60]

Kadiri mja anavyohitaji msaada na kujikurubisha karibu na Allaah ndivyo du’aa yake inavyopokelewa.
Hadiyth uliyoitaja ni dhaifu kwa sababu (katika wapokezi kuna) Marwaan bin Saalim Al-Muqfayaa hajulikani.


[Ithaaf Al-Kiraam bi-Ajwibati Ahkaami Az-Zakaat wal-Hajj wasw-Swiyaam]

0 Comments